Jumatatu, 30 Machi 2015

sababu za kuanzishwa kwa nadharia za fonolojia



Massamba (2011:2) anasema “Nadharia yoyote mpya hujaribu kuboresha hiyo ya zamani”, Hakuna  nadharia mpya inayozuka katika ombe tu.
Kwa mtazamo huo, nadharia mpya huzaliwa kwa sababu za kuutafiti, kujaribu dhana na kutokea kwa matukio kadhaa katika maisha. Insha hii itajikita kwa ufupi katika kupitia nadharia za    wanamuundo(wanatakisonomia),wanafonolojia zalishi na nadharia ya wanafonolojia vipande sauti huru ili  kujua sababu zilizopelekea kuanzishwa kwa nadharia ya fonolojia.
Nadharia ya wanataksonomia hawa ni wanafonolojia wa mwanzoni  Miongoni mwa waasisi wa nadharia hii ni pamoja Jan Baudeuin de Courtenay(1845-1929), Ferdinand de Saussure (1857-193), Prince Nikolaj Sergeevic Trubetzkoy(1890-1939), Daniel Jones (1881-19670, Edward Sapir 91884-1939) na Leonard Bloomfield (1887-1949.Ilijishughulisha na kuchunguza mabadiliko ya miunganiko ya sauti yanayojitokeza katika mofimu zinapoungana.Kuchunguza mabadiliko ya sauti yenye kazi ya kimofolojia,vile vile walijaribu kuelezea namna ambavyo maneno ya lugha yanayotamkwa yangeweza  kugawanywa katika makundi mawili,(yaliyopo akilini mwa msemaji na maneno yenyewe yanayo tamkwa),pia kuyagawa na kuyaainisha maumbo kivipande vipande na warijaribu kutafuta mbinu au utaratibu katika kuzibaini fonimu za lugha yeyote ya binaadamu.Ingawa uchanganuzi ulikuwa ukiainisha maumbo mbalimbali ya sauti au mofu zilizokuwa zikihusiana kimaana au kiamilifu lakini hawakuonesha uhusiano huo baina ya maumbo hayo.Chomky na Halle wakaona ni vipi tunaweza kuyahusisha maumbo hayo ndipo nadharia ya kiunzi rasmi cha  fonolojia zalishi  ikatokea ili kupunguza tatizo hilo.
Waasisi wa nadharia hii ni Noam Chomsky na Morris Halle.  Wamefanya uchanganuzi wa vipengele vya kifonolojia katika kitabu chao.  “The Sound Pattern of English” (1968).Kiunzi hiki kinadharia kimejengwa kwenye misingi mikuu mitatu yaani umbo la ndani ambalo hujengeka katika akili ya msemaji,umbo la nje huwakilisha maneno tutamkayo katika vinywa vyetu na sauti zote zitumikazo katika lugha asilia ya binaadamu hutokana na mifumo ya mkondo hewa ambayo ama inakwenda ndani au inatoka nje.pia matumizi sahihi ya sheria ni jambo lililotiliwa mkazo na kiunzi rasmi cha fonolojia zalishi.
Kwa mujibu wa Massamba (2011:108) anasema Kiunzi cha fonolojia zalishi kinawakilisha vipengele mbalimbali vya kifonolojia kiulalo unaojulikana kama uwakilishi moza (uwakilishi mkururo) yaani kila kipengele kichambuliwe kisanjari  na hivyo kuchukulia vipamba sauti kama ni  vijenzi vya vitamkwa.
Mkabala wa Chomsky na Halle ulichanganua vipengele vyote vya fonolojia kimoza.  Vipengele.walichukulia vipambasauti vyote kama mkazo,toni,usilabi ni sahemu ya viambajengo vya kitamkwa kinachohusiana  navyo. Mfano katika neno mẽmã:
                        M                                           m                    
                   +midomo              -nyuma           
                  +konsonanti                        - mviringo
                   +unazali                -juu
                  +korona                 +vokali
                                                +nazali
Hii ina maana kuwa irabu inakuwa na sifa ya unazali kwa sababu inaambukizwa unazali na konsonanti ya nazali iliyoambatana nayo.
                       
Kama mfano unavyoonesha hapo juu katika uchanganuzi wa vipengele vya kifonolojia, vipambasauti vinachukuliwa kuwa ni sehemu ya kitamkwa. Hivyo kusababisha kuwa na irabu yenye unazali na e isiyo na unazali. Kitu ambacho si sahihi katika lugha ya Kiswahili.

Kwa msingi huu kama unazali unachukuliwa kuwa ni sehemu ya kitamkwa e mbona katika maneno mengine haiwi na unazali? Mfano katika neno pema.

Pia tatizo linakuwepo katika uwakilishi wa toni kwa lugha zenye toni, toni huwa inahama kutoka kwenye silabi moja kwenda kwenye silabi nyingine, mfano katika kimakonde
                          Kimakonde                  Kiswahili     
                        Anίida                          – amekuja
                        Aniida kύkaya                        – amekuja nyumbani
Toni juu inaonekana imehama kutoka katika irabu  i  katika silabi  ni  kwenda kwenye irabu  u  katika silabi ku. Hivyo kusababisha  i  katika silabi   ni  kupoteza sifa ya toni juu. Swali la kujiuliza kama toni juu ni sifa ya irabu hiyo kwa nini isiendelee kuwa nayo sifa hiyo?

Vilevile uwakilishi wa mkazo katika lugha imeonekana kuwa ni tatizo, mfano katika tungo mtoto, huwa kwa kawaida katika lugha ya Kiswahili mkazo huwekwa katika silabi ya pili kutoka mwisho. Hivyo tunakuwa na:
            m          toto                        (  +mkazo)
Hapa silabi to ina mkazo kwa kuwa ndio silabi ya pili toka mwisho mwa neno hilo, lakini tunapoongeza neno mbele ikawa mtoto mzuri mkazo unahama kutoka katika silabi to katika neno mtoto kwenda katika silabi zu katika neno mzuri. Sasa tujiulize kama mkazo ni sifa ya silabi to katika neno mtoto, kwani nini sifa hiyo ipotee kwenda katika silabi zu? Kwa nini isiendelee kubakia katika silabi to? Hili ni tatizo.

Pia katika uwakilishaji wa usilabi katika lugha ya Kiswahili. Neno mti asili yake ni muti, ambapo neno hilo huchukuliwa kuwa na silabi mbili yaani mu na ti. Na kilele cha silabi huwa ni irabu. Neno muti  hutamkwa mti ambapo irabu u hudondoshwa ambayo ndiyo kilele cha usilabi katika silabi mu, lakini bado usilabi unabakia katika konsonanti m. Kama usilabi ni sifa ya irabu u nayo imedondoshwa, kwani nini usilabi uendelee kubakia katika konsonanti m? pia inaonekana kuna tatizo.

Kutokana na ukweli kwamba sifa za toni, usilabi, mkazo na unazali katika lugha inaonesha kutohusiana moja kwa moja na vitamkwa, kwani kitamkwa fulani kinaweza kudondoshwa lakini sifa hiyo inahamia katika kitamkwa kingine
Kutokana na matatizo ya uwakilishi wa vipengele mbalimbali vya kifonolojia katika nadharia ya fonolojia zalishi wataalamu wengine waliibukia na nadharia yao ili kuweza  kurekebisha matatizo hayo.
Goldsmith (1977) alikuja na  nadharia ya fonolojia vipande sauti huru ambapo kila kitamkwa kilichukuliwa katika rusu zinazojitegemea.Pia (1975:176) ameeleza kuwa ni nadharia ambayo ilianzishwa kwa ajili ya kuondoa tatizo ambalo  lilikuwepo baada ya nadharia ya fonolojia zalishi.

Fonolojia  vipandesauti  huru (Autosegmental pholology) ni  mtazamo wa kinadharia katika uchanganuzi wa mfumo wa sauti za  lugha asilia ambazo umekitwa katika msingi kwamba kila kipande sauti (kitamkwa, mkazo, toni) hujitegemea na  huwa  katika rusu yake chenyewe (si sehemu ya kingine) Massamba (2009:13).
Vipengele vya kifonolojia vichanganuliwe kwa kutumia uwakilishi rusu.  Rusu hizo huwakilishwa kwa kutumia  mistari ya uhusiano inayodhibitiwa na sharti la ukubalifu (Goldsmith 1976:27) sharti la  ukubalifu lina kanuni tatu:
  • Kila toni ihusishwe na angalau irabu moja
  • Kila irabu ihusishwe na angalau toni moja
  • Mistari ya uhusiano isikingamane,mfano kutoka  kimakonde
           *                         Rusu ya kiinitoni(RVt)
              Ku   kί     mbi    la        Rusu ya vitamkwa (RV)

                                                 Mistari ya uhusiano (MU)
              C    J            C              Rusu ya toni(RT)         
                                                                                                                                                                                          
Pia kufanya uchanganuzi wa Kupunguza sheria zinazobadili sifa na kutumia kanuni zinazodondosha au kupangilia upya vipandesauti kwa kutumia njia ya kurekebisha mistari ya uhusiano.
Kwa kuhitimisha kiunzi cha  fonolojia zalishi  iliibuka kwa kutokana na udhaifu au uliotokana na wanataksonomia na fonolojia vipande sauti huru iliibuka kutokana na matatizo ya fonolojia zalishi  ambao waliamini kuwa vipambasauti ni vijenzi vya vitamkwa.japo kuwa wote  wanaongelea umbo la nje na la ndani katika kuchambua fonimu katika lugha na sheria na utaratibu zisizo badilifu

                                        MAREJELEO

Massamba. D.P.B,( 2012) Misingi ya fonolojia,TATAKI ,Dar es salaam
Massamba .D.P.B. (2010) Phonological Theory History Studies and development:  Institute of Kiswahili Studies, Dar es Salaam

Massamba (2011) Maendeleo katika nadharia ya fonolojia  TATAKI, Dar es Salaam


Maoni 7 :

  1. uuuuuiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii

    JibuFuta
  2. ni vyema zaidi sisi kama wanazuoni kufanya tafiti zaidi katika suala zima la kukuza na kukipaumbele kiswahili ili kuleta tija zaidio kwa maendeleo ya taifa letu na kupanua wigo wa ajira kupitia lugha yetu ya kiswahili

    JibuFuta
  3. Eleza kaa mfano mahususi jinsi makundi makuu ya sauti yanayojitofautiana Kaa mujibu wa NOAM CHOMSKY na Moriss HALLE

    JibuFuta
  4. Eleza kaa mfano mahususi jinsi makundi makuu ya sauti yanayojitofautiana Kaa mujibu wa NOAM CHOMSKY na Moriss HALLE

    JibuFuta
  5. Eleza kaa mfano mahususi jinsi makundi makuu ya sauti yanayojitofautiana Kaa mujibu wa NOAM CHOMSKY na Moriss HALLE

    JibuFuta
  6. Asante kwa kazi mzuri munayoifanya. Nawaomba muendelee hivyo hivyo kwani munatusaidia sana sisi wanafunzi wa isimu katika vyuo vikuu

    JibuFuta